Thursday, 4 December 2014

Mwanafunzi aliyekua ana nadi ubikra akoma

Mwanafunzi anayesomea udaktari nchini Marekani ambaye alikuwa ana nadi ubikra wake, amesitisha shughuli hiyo baada ya watu wachache sana kujitokeza wakiwa tayari kuulipia ubikra wa mwanamke huyo.
Pamoja na hilo Kern hakua na uhakika kuhusu ukweli wa waliojitokeza kulipia ubikra wake.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa jarida la Daily Mail.
Mwanafunzi huyo, Hanna Kern alikuwa ana nadi ubikra wake chini ya jina ambalo sio lake 'Elizabeth Raine' kwa hofu ya watu kumtusi. Pia hakuweka sura yake kwenye mtandao hadi alipofanya mahojiano na jarida la Haffington post.
Kern ana umri wa miaka 28 na ana digrii ya uzamifu kutoka chuo kikuu cha Washington, nchini Marekani.
Kern ni mwanafunzi wa hivi karibuni aliyenadi ubikra wake kwenye mtandao bila matokeo aliyoyataka.
Hata hivyo alilazimika kuusitisha mnada wake baada ya kukosa kupata kima alichokitaka na hata pia kukosa kupata wanaume wengi waliovutiwa na kampeini yake na kuhofia kuwa waliojitokeza kuulipia sio watu wakweli.
Pia alieleza kuwa alisumbuka sana kiakili kutokana na umaarfu aliopata baada ya kufichua jina lake la kweli na kuonyesha sura yake.
Alikunukuliwa akisema baada ya kukosa kufanikiwa kupata hela alizozitarajia, hana wasiwasi na hilo kwani amapeta funzo na kujua kwa nini kampeini kama hizi huwa kazifanikiwi.
Wa mwisho aliyejitokeza kulipia ubikra wake alikuwa ametoa kima cha dola 801,000,lakini mwanafunzi huyo aliamua kutoendelea na juhudi zake kwani hakufurahishwa na pesa hizo.
''Nimeamua kusitisha kempeini yangu, na kurejea katika msomo yangu ya udaktari.''
''Bado ninaamini kuwa ubikra ni kitu kizuru na pia ninaamini kuwa mwanamke anapaswa kuachwa afanye anavyotaka, '' ingawa kwa sasa masomo ndio ninayotaka kushughulika nayo,'' alisema Kern.

Serekuma atua rasmi Simba Sc

Mshambuliaji matata wa kilabu ya Gor Mahia nchini Kenya Dan Sserenkuma aihama kilabu ya Simba SC

Aliyekuwa Mshambuliiaji wa mabingwa wa soka nchini Kenya Gor Mahia Dan Serenkuma amejiunga na kilabu ya Tanzania Simba SC.
Raia huyo wa Uganda alijiunga na kilabu hiyo ya Ligi ya Vodacom na kutamatisha kazi yake ya miaka mitatu katika ligi ya Kenya ambapo alianza kwa kuichezea Nairobi City Stars kabla ya kujiunga na Gor ambapo alikuwa kiungo muhimu katika ushindi wa ligi mara mbili.
''Nimefurahia miaka miwili na nusu katika kilabu ya Gor Mahia,lakini huu ndio wakati muhimu wa kuaga.Tumefurahia nyakati maalum na mafanikio pamoja,na habiki wamenisaidia sana hususan wakati mgumu'',Mfungaji huyo wa mabao mengi katika ligi ya Kenya aliandika katika mtandao wake wa Twitter.
''Ningependa kumshukuru kila mtu katika usimamizi wa kilabu kwa kunipa fursa muhimu ili kuonyesha kipaji changu.
Dan Sserenkuma
Mchezaji huyo wa kimataifa katika timu ya Uganda Cranes alipigwa picha katika mtandao wa kilabu hiyo akifanyiwa majaribio pamoja na kupimwa afya na sasa anatarajiwa kujiunga na wachezaji wenzake katika barabara ya Msimbazi mjini Daresalaam tayari kwa maandalizi ya mechi za ligi ya Tanzania.
Wakati huohuo imebainika kwamba Kilabu ya Gor Mahia ilishindwa kumzuia mchezaji huyo.
Duru zimearifu kuwa mchezaji huyo aliandamwa na kilabu ya Gor mahia kufuatia ripoti za vyombo vya habari kwamba alitarajiwa kujiunga na Simba.
Lakini Gor Mahia haikuwasilisha ombi lolote la fedha kwa kuwa mchezaji huyo tayari alikuwa ameweka kandarasi yenye thamani ya shilingi millioni 3 pamoja na mshahara wa ksh.250,000 kwa mwezi na kilabu hiyo ya Tanzania ambapo atajiunga na mchezaji mwengine wa Gor Mahia Mungai Kiongera.

Lungu ndiye mgombea wa PF Zambia

Mahakama kuu nchini Zambia imetangaza kuwa waziri wa Ulinzi Edgar Lungu ndio atakeyewania wadhfa wa Urais kupitia tiketi ya chama cha Patriotic Front katika uchaguzi wa mwezi Ujao.
Chama cha Patritic Front kimegawanyika kuhusu ni nani atakayekrithi rais sata kufuatia kifo chake.
Mgawanyiko huo utafungua njia kwa upinzani kuchukua mamlaka katika uchaguzi huo kulingana na wachambuzi.
Makundi pinzani ya chama cha PF yalifanya mikutano tofauti katika kipindi cha juma moja ili kumchagua mgombea wa urais katika uchaguzi huo wa january 20.
Upande wa bwana Lungu ulipinga uteuzi wa Bwana Sampa mahakamani.
''Mkutano wa chama unaodaiwa kufanyika Disemba mosi ambapo mheshimiwa Miles sampa anadaiwa kuchaguliwa kama mgombea wa chama cha Patritic Front nataka kutangaza kwamba ni haramu na uamuzi wote ulioafikiwa si wa halkali'',Jaji aliamuru.
Kaimu rais wa Zambia Guy Scott
Bwana sampa amesema kuwa atakataa rufaa dhidi ya uamuzi huo.
Kiongozi huyo ni mshirika wa karibu wa kaimu rais Guy Scott ambaye alichungua mamlka baada ya kifo cha Sata katika hospitali ya Uingereza mnamo mwezi Octoba akiwa na umri wa miaka 77.
Bwana Scott alichukua jukumu muhimu katika mgogoro wa kuwania mamlaka alipomuondoa kwa mda bwana Lungu kama katibu mkuu wa chama hicho mda mchache baada ya kifo cha Sata.
Hatahivyo alilazimika kurudisha bwana Lungu siku moja baadaye kufuatia lalama katika chama.
Bwana Scott ambaye hawezi kupigania urais anajaribu kuwa mtu muhimu katika siasa za taifa hilo kulingana na wachambuzi..

Mama matatani kwa kumpa mwanae Bangi Nchin Canada

Mama wa kijana anayeugua kifafa amekataa kumpa mwanawe wa kiume bangi kama matibabu inavyotakikana-kupitia moshi na mvuke. Mtoto huyo anapasawa kutumia Bangi kama dawa kupambana na ugonjwa wake wa Kifafa kwa maagizo ya daktari.
Liam McKnight mwenye umri wa miaka sita napenda kucheza na ndiye wa kwanza kila mara kukimbia kuelekea mlangoni.Mamake mzazi,Mandy,anasema kuwa mwanawe anapenda kujua nani anawatembelea.
Familia hiyo ya McKnight inayoishi jijini Otawa nchini Canada ina wageni wengi wanaowatembelea-kutoka kwa wanachama wa kukindi cha densi anachoshiriki binti yao,na hata wauguzi wa kutamka,wa kunyosha viungo vya mwili,wataalam wa kusikiza-wote wanaomtembelea Liam.
Liam ana ugonjwa unaojulikana kama Dravet ambayo,ni aina kali sana ya kifafa.Afya yake hudhoofika mara kwa mara lakini baada ya kufanyiwa majaribio kadha wa kdha ya matibabu ya ugonjwa huo, anglau hali yake imeimarika kidogo.
Mamake Liam humpa mafuta ya Bangi, ambayo yemtolewa kwa sehemu changa sana ya mmea huo.
Mwezi Juni mwaka huu,siku kabla Liam kuanza kutumia mafuta hjayo ya Bangi,(iliyotengezwa kutoka kwa aina ya bangi yenye ufanisi) alizirai kama mara 67. Katika siku kumi zilizofuatia alizirai tu mara moja.
Nchi nyingi duniani zinakabiliwa na changamoto za kuidhinisha matumizi ya Bangi.
Tatizo ni kuwa matibabu ya Liam ni haramu. Kutumia dawa inayotengezwa kwa Bangi inakubalika Canada lakini lazima iwe tu majani ya Bnagi yaliyokaushwa au mvuke wa majani hayo.
Kwa Mandy hilo haliwezakni kwa mwanawe kuvuta moshi wa Bangi akiwa umri huo mdogo.
Matoto mdogo anawezaje kuvuta Bangi? anauliza mamake Liam.
Mapema mwaka 2001, Canada iliruhusu wagonjwa wanaohisi uchungu mwingi kutumia Bangi kama matibabu. Lakini hakuna majaribio yaliyofanyiwa mafuta ya Bangi kujua usalama wake kwa afya ya mtu.
Liam ana umri mdogo sana lakini anaweza kutumia mvuke wa Bangi lakini mamake Liam anasema vipimo vinyovyofa akwa afya ya Liam ni vya mafuta ya Bnagi.
Mamake Liam aliwahi kuiandikia serikali Barua kuielezea kuhusu masaibu yake kuhusiana na matibabu ya Liam. Lakini waziri wa afya alimjibu kwa kusema anaelewa masaibu ya mtoto Liam wakati akikabiliana na ugonjwa wake hatari wa kifafa. Lakini alisisitiza kuwa hadi leo serikali bado haijaidhinisha matumizi ya mafuta ya Bangi wala uuzaji wa mafuta hayo nchini Canada.
Matumizi ya mafuta ya Bangi, yaliruhusiwa mjini Minnesota Marekanimwezi Mei, lakini sheria hiyo haitaanza kutumika hadi Julai mwaka 2015.
Sheria za Bangi kote duniani zinatofautiana.
Mamake Liam anafahamu kuwa anavunja sheria pamoja na kufahamu athari z akutumia mafuta ya Bangi. ''Je nahofia kuwa navunja sheria? ndio. Lakini nahofia zaidi ikiwa hatutafanya chochote hali ya afuya ya mtoto wangu itazorota.
Kwetu Mafuta ya Bangi ndio tiba anayohitaji mwanangu. Hatukuwa na mda wa kusubiri majaribio kufanywa. Kwa kila siku, Liam hula kijiko kimoja cha Bangi ikiwa imechanganywa na mafuta ya nazi.

Chelsea,Arsenal na man city zafanya mauaji Epl

Mzunguko wa 14 umekamilika kwa timu zote 20 za ligi kuu ya England kushuka viwanjani.
Chelsea, wameendeleza wimbi la ushindi na kukataa katakata kuzipa nafasi timu nyingine 19 kupunguza pengo la pointi lililopo kati yake na timu hizo.
Sergio Aguero, mchezaji wa Manchester City akishangilia moja ya magoli yake katika ligi kuu ya England
Chelsea imeendelea kuwa na tofauti ya pointi sita na Man City inayoifuatia baada ya kuirarua Tottenham mabao 3-0, huku Manchester City yenye pointi 30 ikiisasambua Sunderland magoli 4-1. Sergio Aguero ameifungia timu yake ya Manchester City magoli mawili katika mchezo huo, huku Jovetic na Zabaleta kila mmoja akifunga bao moja.
Magoli ya Chelsea yamefungwa na Hazard, Drogba na Remy.
Wachezaji wa Arsenal Santi Carzola akishangilia goli na Alexis Sanchez
Mchezo mwingine wa Jumatano usiku, ulikuwa kati ya Arsenal na Southampton wanaoshikilia nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi kuu ya England. Mchezaji Alexis Sanchez ndiye aliyekuwa shujaa na kuwanyanyua vichwa mashabiki wa Arsenal pale alipoifungia timu yake goli pekee katika mchezo huo ikiwa ni dakika ya 89 ya mchezo, uliofanyika uwanja wa Emirates na hivyo kujikusanyia pointi tatu muhimu kuelekea kileleni.Arsenal inashikilia nafasi ya sita ikiwa na pointi 23, pointi 13 nyuma ya vinara Chelsea yenye pointi 36.
Everton na Hull City ziligawa pointi baada ya kufungana bao 1-1.
Hadi kufikia mzunguko huo wa 14, Chelsea inaongoza kwa kujikusanyia pointi 36, ikifuatiwa na Man City yenye pointi 30, Southampton ni ya tatu na pointi 26, Huku Manchester United kiwa nafasi ya nne na pointi 25 na nafasi ya tano inashikiliwa na West Ham yenye pointi 24.Ivabaada

makundi ya AFCON 2015 haya hapa

Upangaji wa makundi ya timu kumi na sita zilizofuzu kucheza fainali za mashindano ya 30 ya kuwania Kombe la Mataifa ya Afrika kwa mwaka 2015 yamefanyika katika mji mkuu wa Equatorial Guinea, Malabo.
Mashindano hayo yataanza Januari 17, 2015.
Upangaji wa makundi ulirudishwa wiki moja nyuma ili kuiwezesha Equatorial Guinea, kujiandaa baada ya kuchukua nafasi ya Morocco, iliyokuwa iandae mashindano hayo, lakini ilishindwa kufanya hivyo baada ya kutaka mashindano hayo yasogezwe mbele kuhofia ugonjwa wa Ebola ambao umeyakumba baadhi ya mataifa ya Afrika Magharibi, ambako zinatoka timu nyingi zinazoshiriki michuano hiyo.
Mabingwa watetezi Nigeria ni moja ya timu kubwa zilizoshindwa kufuzu kucheza fainali za mwakani, pamoja na Misri na Angola ambazo zote kwa mshangao hazitaweza kushiriki.
Haya hapa makundi manne ya AFCON 2015:
Kundi A Equatorial Guinea, Burkina Faso, Gabon, Congo
Kundi B Zambia, Tunisia, Cape Verde, DR Congo
Kundi C Ghana, Algeria, South Africa, Senegal
Kundi D Ivory Coast, Mali, Cameroon, Guinea
Wenyeji Equatorial Guinea na Congo zitacheza mechi ya ufunguzi wa michuano hiyo. Kundi D ndilo linaloonekana kuwa gumu zaidi kutokana na timu zilizopangwa kundi hilo.

Tuesday, 2 December 2014

Misri yafunga mipaka yao

Misri yafunga lango la mpakani tena
Misri imefunga lango la mpaka wa Rafah unaounganisha nchi hiyo na Gaza
Katika maelezo yaliyoandikwa na Kamati Kuu ya Mipaka na Milango ya mpakani, inayohusishwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya serikali ya Palestina iliyoko Gaza, iliarifiwa kwamba serikali ya Misri ilifunga lango la mpaka wa Rafah hadi amri ya pili itakapotolewa baada ya Wapalestina 554 waliokwama nchini humo kuvuka Gaza.

Viongozi wa Misri waliwahi kufungua lango la mpaka wa Rafah pia siku ya jumatano iliyopita kwa ajili ya Wapalestina waliokuwa wakisubiria kupita Gaza.

Kutokana na vizuizi vya Israel, ‘’Lango la Pekee la Gaza kwa dunia’’ la Rafah limekuwa likifungwa mara kwa mara baada ya mapinduzi ya kijeshi yaliyotekelezwa mwezi Julai 2013 nchini Misri. Hatimaye mnamo tarehe 24 Oktoba, baada ya mashambulizi kutekelezwa katika vituo 2 vya usalama mkoani Sinai Kaskazini, serikali ya Misri ilitoa ilani ya dharura ya miezi 3 kwenye eneo hilo kwa madai ya ‘’kutatua mizizi ya tatizo la ugaidi’’, na kuchukua hatua ya kufunga lango la mpaka wa Rafah katika mchakato huo.