Friday 20 March 2015

Ajali zaendelea kuitesa Tanzania, yaua watu 7

Mchana wa  jana  basi ya RUWINZO DAR kwenda  SONGEA na Basi la IFAKARA EXPRESS yamegongana maeneo ya mikumi. Inasemekana Abiria 7 wamefarik hapo hapo. Tuendelee kuombea Taifa letu .
Image result for ajali ya basi jana  Mwandishi wetu alifanikiwa kuongea na mmoja wa mhanga wa ajali hiyo alisema "Hali halisi ya ajali ni kuwa na mwendo wa kasi dereva wetu tulipofika mikumi majira ya saa 5:30 asubuhi tukitokea dar es salaam kuelekea malininyi-mahenge Gari nililolipanda mimi linaitwa MSANGA line express ambalo linafanya safari zake Dar,ifakara-malinyi tulipofika mikumi mbele yetu kulikuwa na lori lenye namba za usajili  T 299 nalo lilikuwa linatoka dar-iringa dereva wetu alikuwa ana-over take hilo lori kabla hajamaliza kupita hilo lori alikutana  uso kwa uso na basi la ruwenzo ambalo lilikuwa linatoka njombe kuelekea dar sasa dereva wetu akaona amkwepe huyu mwenye basi la ruwenzo anafanya hivyo na ruwenzoakawa ameshaingia kwahiyo  amelipiga kwa nyuma Gari letu na hapo hapo Gari letu kwa sababu lilikuwa na mwendo kasi lilivyopigwa likabilingika Mara moja juu chini alafu likakaa sawa na kuziba njia marehemu nilioshuhudia kwa macho yangu ni 7 majeruhi usiseme wengine wamekatika miguu wangine mikono wangine kichwa vinavuja damu kama maji sasa nilivyokuwa nahojiwa na Mkuu wa polic wa wilaya akapigiwa simu tena kusema waliobebwa Hosp.wamefaliki 3 so ukijumlisha utapata 10 ili kuna uwezekano wa waliofariki wakaongezeka maana  hali zao ni mbaya sana

No comments: