Wednesday 11 January 2017

POLISI WAKAMATA NOTI BANDI ZENYE THAMANI YA SH MIL 8 MKOANI TABORA

Polisi wilayani Igunga mkoni Tabora wamewakamata watu watatu wakiwa na noti bandia za shilingi 10,000 zipatazo mia nane sawa na shilingi milioni nane wakiwa wamezihifadhi kwenye buti ya gari yao ndogo
Watuhumiwa waliokamatwa na noti hizo ni  Luneka Magasha 35) mkazi wa Igunga, Zengo Magasha (25) mkazi wa mkoa wa Lindi na James Hangalu  mkazi wa Dar es salaam
Kamanda wa polisi mkoa wa Tabora Hamisi Selemani alithibitisha kukamatwa kwa watu hao na kusema kuwa polisi walipata taarifa ya kuwepo kwa watu wenye noti za bandia na baada ya taarifa hiyo walikwenda eneo la tukio na kuwakuta watu hao waikiwa na gari ndogo yenye namba za usajili  T 964 BEC

Aidha kamanda Selemani alisema kuwa baada ya kuwapakua kwenye gari yao walikuta shilingi million nane na elfu kumi kwenye buti ya gari hiyo
“Baada ya kuwahoji watu hao walikiri kuwa noti hizo ni zabandia na nimali yao na walikuwa wamejipanga kuzisambaza katika minada ya ng’ombe  ya Igunga na Ibologelo” alisema kamanda selemani
Kamanda aliongeza kuwa fedha hizo pamoja na gari waliokutwa nayo vinashikiliwa na jeshi la polisi, na ametoa wito kwa wananchi kuwa makini katika biashara zao na kwenye magulio mbalimbali mkoani humo.

No comments: