Tuesday 24 January 2017

Wafungwa zaidi a 300 waachiliwa huru Bujumbura

Wafungwa zaidi ya 300 wameachiliwa huru hii leo kwenye jela kuu ya Mpimba Bujumbura, likiwa ni zoezi la kupunguza msongamano katika magereza mbali mbali nchini humo. Hatua hiyo ni katika utekelezaji wa msamaha wa rais Pierre Nkurunziza. Miongoni mwa walioachiwa huru ni pamoja na wale waliopatikana na hatia ya kujihusisha na vugu vugu la kupinga muhula wa 3 kwa rais huyo. Kuachiliwa wafungwa hao pia ni moja ya vigezo vilivyoowekwa na Umoja wa Ulaya ili irudi kuisaidia kifedha Burundi.

No comments: