SERIKALI imesema kama Shirika la Afya Duniani (WHO),
litapitisha matumizi ya dawa mpya ya ugonjwa Ukimwi wataitumia, lakini
kwa sasa haiwezi kuzungumzia tafiti za ugonjwa huo ambazo zipo nyingi.
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto, Michael John, amesema kwa sasa zipo tafiti
nyingi, lakini wao kama wizara wanasubiri mwongozo kutoka WHO ambao
ndiyo unathibitisha ubora wa dawa na matumizi yake.
“Zipo tafiti nyingi tunazisikia zinafanyika, lakini hili la
Ukimwi ni mapema mno kulizungumzia ila kinachohitajika ni kusubiri
mwongozo wa WHO ambao ndio wanatuongoza kwenye orodha ya dawa na
matumizi yake katika magonjwa mbalimbali,” alisema John.
Hatimaye baada ya danadana za muda mrefu, uchaguzi wa
kuwachagua Mameya wa Manispaa za Kinondoni na Ilala, umefanyika na Umoja
wa Vyama vinavyunda Katiba ya Wananchi (Ukawa) wamefanikiwa kuongoza
Manispaa hizo.

Manchester United wanajiandaa kutoa pauni milioni 140, ili kutengua
kigezo cha uhamisho cha Neymar, 23 anayeichezea Barcelona, baada ya
mazungumzo ya mkataba mpya kusuasua (Le Sport10), Manchester United
watamruhusu kiungo wao Nick Powell, 21 kwenda kwa mkopo katika timu moja
ya ligi daraja la kwanza (Sun), Southampton hawatomuuza Sadio Mane, 23
au Victor Wanyama, 24 katika dirisha la usajili ya Januari (Times),
