Monday 21 March 2016

Azam yaendeleza Kichapo dhidi ya Bidvest ya afrika Kusini

TIMU ya Azam FC leo imefanikiwa kusonga mbele katika michuano ya Kombe la Shirikisho baada ya kuifunga Bidvest Wits ya Afrika Kusini kwa mabao 4-3 kwenye mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Chamazi jijini Dar.

Mabao ya Azam FC yamepachikwa kimiani na Kipre Tchetche aliyefunga mabao matatu ‘hat trick’ na moja likapachiwa na nahodha wa timu hiyo, John Bocco.

Katika mechi ya kwanza, Bidvest ilipoteza kwa mabao 3-0 ikiwa nyumbani Johannesburg. Safari hii imepata mabao matatu lakini ikashindiliwa mengine manne. Maana yake Azam FC imevuka kwa jumla ya mabao 7-3

No comments: