Sunday 30 March 2014

CHELSEA ya lala MAN U yaona mwangaza

Matumaini ya kuchukua ubingwa wa ligi kuu soka nchini England kwa Chelsea yamedidimia baada ya kujikuta wakipoteza mchezo wao dhidi ya Crystal Palace kwenye uwanja wa Selhurst Park.

Crystal Palace maarufu kama The Eagles wameishangaza Chelsea kwa kipigo cha bao moja, bao ambalo nahodha wa Chelsea John Terry alijifunga mwenyewe baada ya klosi ya Joel Ward.

Shukhrani ziende kwa mlinda mlango wa Palace Julian Sperioni ambaye aliokoa michomo miwili ya Edin Hazard na nafasi ya wazi ya John Terry ambaye alikuwa asawazishe.

Cameron Jerome alimanusra afanye matokeo yawe 2-0 baada ya shuti lake kugonga mwamba na kuokolewa.

Ushindi wa Palace ni wa kwanza katika mechi sita za ligi kuu na zinakifanya kikosi cha kocha wake Tony Pulis kusogea kwa pointi tano kutoka katika timu tatu zilizo katika hatari ya kushuka daraja.

Huku chelsea ilkilala 1 0 Manchester United imeona mwanga kwa kuichapa Aston Villa 4 1
Wayne Rooney akifunga bao la kwanza la United ikicheza na Aston Villa.
Kwingineko Manchester United ilishinda katika mechi yake ya mapema kwa mabao 4-1 dhidi ya Aston Villa.

Wayne Rooney alifunga mabao mawili huku Juan Mata na Javier Hernandez wakifunga kuhutimisha ushindi mkubwa wa wiki kwa David Moyes ambaye leo alikumbana na bango nje ya uwanja wa Old Traford kumtaka aondoke.

Manchester United watapambana na Bayern Munich katika mchezo wa robo fainali michuano ya klabu bingwa barani Ulaya hapo siku ya jumanne.

Southampton wakaiadhibu Newcastle kwa mabao manne kwa sinia kwenye uwanja wa St.Marys.

The Saints ambayo ina washambuliaji muhimu wanaotegemewa na kocha wa timu ya taifa ya England,leo kwa mara nyingine walionyesha matumaini ya waingereza kuwa na wachezaji wazuri kwenye safu ya ushambualiaji kwani magoli yote yalifungwa na washambuliaji wa England Jay Rodriguez, Rickie Lambert na Adam Lallana.

Nayo Stoke City waliichapa Hull City 1-0.

Swansea wakaiadhibu Norwich kwa mabao 3-0 huku majirani zao Cardiff City wao wakaponea kwa sare ya 3-3 ugenini walipokuwa wageni wa West Brom kwenye uwanja wa The Hawthorns

No comments: