Monday 17 March 2014

Chadema yafa kiume kalenga

Polisi akilinda Kituo cha Kupigia Kura cha Shule ya Chekechea ya Mchwivila katika Jimbo la Kalenga, Iringa jana

Mgombea wa CCM, Godfrey Mgimwa anaonekana kufanya vizuri katika uchaguzi mdogo wa ubunge uliofanyika jana katika Jimbo la Kalenga, mkoani Iringa.

Mgimwa aliwaacha mbali mshindani wake wa karibu, Grace Tendega wa Chadema na Richard Minja wa Chausta.

Kutokana na hali hiyo, wafuasi wa CCM katika sehemu mbalimbali za jimbo hilo na Mjini Iringa walikuwa wakishangilia kile walichokiita ushindi wa kishindo.

Watu 71, 765 walitarajiwa kupiga kura katika vituo 216, lakini waandishi wa Mwananchi walisema kulikuwa na idadi ndogo ya watu waliojitokeza katika baadhi ya vituo, huku wengi wakilalamika kushindwa kupiga kura kutokana na kupoteza vitambulisho.

Vituo vya kupigia kura vilifungwa saa 10:00 na kazi ya kuhesabu kura ilianza mara moja na matokeo yalianza kubandikwa kwenye vituo husika kuanzia saa 11:00 jioni huku CCM kikionekana kufanya vizuri kuliko vyama vingine.

Msimamizi wa Uchaguzi, Jimbo la Kalenga, Purdenciana Kisaka alisema uchaguzi ulifanyika kwa ufanisi... “Mimi na timu yangu hivi sasa tunajiandaa kupokea masanduku ya kura, ili tujumlishe na kuona kile kilichomo. Tutatangaza matokeo mapema kadiri inavyowezekana,” alisema Kisaka.

Matokeo ambayo yalikuwa yamebandikwa vituoni na kunukuliwa na waandishi wetu ni kama ifuatavyo:

Kata ya Ifunda:

Kituo cha Zahanati ya Kibena na. 1; CCM 93, Chadema 36, Chausta 2, Zahanati na.2: CCM 91, Chadema 28, Chausta 0, Shule ya Msingi Kibena CCM 91, Chadema 23, Chausta 0, Ofisi ya Kijiji Ifunda A; CCM 84, Chadema 73, Chausta 1, Kituo B; CCM 75, Chadema 76, Chausta 0.

Kituo cha Kivalali Nyumba ya Mifugo na. 2; CCM 109, Chadema 14, Chausta 1, Kivalali na. 1: CCM 99, Chadema 19, Chausta 1, Kilimahewa B Ofisi ya Kitongoji; CCM 57, Chadema 32, Chausta 1.

Kata ya Maboga:

Kijiji cha Makongati Kituo cha Josho, CCM 120, Chadema 13, Chausta 1, Shule ya Msingi Makongati; CCM 160, Chadema 9, Chausta 2,Kijiji cha Kiponzelo, Kituo cha Msombe; CCM 98, Chadema 13, Chausta 0, Shule ya Msingi Kiponzelo; CCM 45, Chadema 5, Chausta 1.
Ofisi ya Kijiji; CCM 231, Chadema 18, Chausta 1, Ofisi Baraza; CCM 207, Chadema 8, Chausta 1, Kijiji cha Magunga, Shule ya Msingi; CCM 180, Chadema 02, Chausta 0, Jengo la Josho Magunga; CCM 184, Chadema 4, Chausta 1

Kata ya Mgama:

Shule ya Msingi Katenge na 1; CCM 90, Chadema 23, Chausta 0, Katenge na 2; CCM 92, Chadema 28, Chausta 1, Shule ya Msingi Mgama; CCM 122, Chadema 40, Chausta 1, Zahanati ya Ihemi; CCM 117, Chadema 67, Chausta 1, Ofisi ya Kijiji Ihemi; CCM 117, Chadema 53, Chausta 0, Mgama Zahanati; CCM 110, Chadema 38, Chausta 0.

Ofisini Mgama; CCM 109, Chadema 44, Chausta 0, Kituo cha Mawasiliano; CCM 97, Chadema 27, Chausta 0.

Kata ya Kiwele

Shule ya Msingi Itagutwa; CCM 105, Chadema 39, Chausta 2, Itagutwa Ofisini; CCM 88, Chadema 43, Chausta 1, Itangutwa Kipengele; CCM 90, Chadema 60, Chausta 2, Malamba B; CCM 148, Chadema 21, Chausta 1, Godauni; CCM 79, Chadema 65, Chausta 1, Ofisi ya Kijiji Kiwele; CCM 99, Chadema 39, Chausta 3.

Shule ya Msingi Kiwele; CCM 61, Chadema 30, Chausta 0, Matembo; CCM 47, Chadema 7, Chausta 0, Mfyome Godauni; CCM 143, Chadema 29, Chausta 0.

Shule ya Msingi Mgera; Chadema 108, CCM 42, Chausta 0, Kidete; CCM 43, Chadema 38, Chausta 1, Mapinduzi; CCM 96, Chadema 65, Chausta, Kidete Ofisi ya zamani; CCM 142, Chadema 58 na Chausta 1.

Kata ya Lumuli

Kituo cha Shule ya Msingi Muwimbi; CCM 164, Chadema 22, Chausta 1, Ofisi ya zamani Muwimbi; CCM 116, Chadema 10, Chausta 0, Shule ya Msingi Muwimbi ‘B’; CCM 87, Chadema 11, Chausta 0, Shule ya Msingi Kitapulimwa; CCM 52, Chadema 58, Chausta 0.

Kata ya Nzihi

Kijiji cha Magubike Kituo Ibogo A; CCM 88, Chadema 19, Chausta 1, Ibogo B; CCM 107, Chadema 15, Chausta 1, Kijiji cha Kidamali A; CCM 91, Chadema 76, Chausta 0, Kidamali B; CCM 94, Chadema 52, Chausta 0, Kijiji cha Nyamihuu, Ofisi ya Kijiji A; CCM 80, Chadema 38, Chausta 0, Kituo B; CCM 58
Nyamihuu Shuleni; CCM 44, Chadema 33, Chausta 0, Nzihi Katani A; CCM 112, Chadema 34, Chausta 1, Kituo B; CCM 116, Chadema 32, Chausta 2,

Kata ya Wasa

Kijiji cha Usengelindete, Zahanati; CCM 260, Chadema 46, Chausta 1, Shule ya Msingi Usengelindete; CCM 116, Chadema 7, Chausta, Kijiji cha Mahanzi, Ofisi ya Kijiji; CCM 130, Chadema 46, Chausta 2, Mahanzi, Ofisi ya Kijiji; CCM 130 Chadema 46, Chausta 2.

Ofisi ya Kijiji cha Mahanzi; CCM 130, Chadema 46, Chausta 2, Ofisi ya Kijiji cha Wasa 1; CCM 149, Chadema 15, Chausta 0, Ofisi ya Wasa 2; CCM 82, Chadema 16, Chausta 0.

Kata ya Luhota

Ofisi ya Kata Luhota; CCM 114, Chadema 48, Chausta 1, Matema Moja; CCM 111, Chadema 34, Chausta 2, Shule ya Msingi Kilambo; CCM 96, Chadema 49, Chausta 2.

Kata ya Kalenga

Chekechea Masukanzi na.2; Chadema 11, CCM 40, Chausta 1, Tosamaganga 1; CCM 3, Chadema 2, Chausta 0, Ofisi Tarafa ya Kalenga; CCM 106, Chadema 26, Chausta 0, Ofisi ya Kijiji cha Kalenga no 1; CCM 134, Chadema 34, Chausta 1, Ofisi ya Kijiji na.2; CCM 168, Chadema 34, Chausta 0.

Kata ya Ulanda

Ofisi ya Kijiji Ibangamoyo CCM 119, Chadema 43, Chausta 1, Mangalali; CCM 196, Chadema 37, Chausta 1, Kituo cha Mwika; CCM 60, Chadema 13 na Chausta 0.

Kata ya Lyamgungwe

Shule ya Msingi Lyamgungwe; CCM 142, Chadema 12 na Chausta 1.
Kata ya Mseke

Kijiji cha Kilindi; CCM 69, Chadema 23, Chausta 23.

Mbali ya kata hizo, habari zilizopatikana wakati tukienda mitambo zilisema CCM ilikuwa ikiongoza katika kata nyingine nyingi.

Awali

Uchaguzi huo uliambatana na matukio kadhaa likiwamo la kukamatwa kwa Msimamizi wa Kituo cha Zahanati ‘B’ katika Kata ya Magulilwa, Benjamin Charles (60) akituhumiwa kumpa karatasi mbili za kupigia kura mpiga kura, Michael John wa Kitongoji C.

Kisaka alisema baada ya msimamizi huyo kukamatwa, alituma msimamizi wa akiba kuendelea na kazi.

“Nimemtuma mwanasheria wetu akaangalie hilo tatizo, suala kama hili tunalifanyia kazi kama tatizo binafsi la msimamizi, kwa hiyo baada ya mwanasheria kurejea tutajua kilichotokea lakini taratibu za kisheria zitachukua mkondo wake,” alisema Kisaka.

Imeandikwa na Geofrey Nyang’oro, Beldina Majinge, Rose Mnyeti, Shaman Lupimo, Hawa Kalinga, Hakimu Mwafongo, Zainab Maeda, Clement Sanga na Saidi Ng’amilo.

No comments: