Monday 31 March 2014

Waandishi wa Al jazeera wanyimwa dhamana

waandishi walionyimwa dhamana

Kesi dhidi ya wandishi watatu wa shirika la habari la Al Jazeera nchini Misiri imeanza kusikilizwa tena leo nchini Misri .

Watatu hao wanatuhumiwa kwa madai ya kusambaza habari za uongo na kusaidia kundi la kigaidi la Muslim brotherhood lililopigwa marufuku.

Waandishi hao ni pamoja na aliyekuwa mwandishi wa habari wa BBC, Peter Greste na Mohamed Fahmya ambaye alikuwa afisa mkuu wa Al Jazeera mjini Cairo.

Watatu hao waliruhusiwa kuongea na jaji ana kwa ana kwa mara ya kwanza tangu wazuiliwe.

Greste alimwambia jaji kuwa hawezi hata kutamka neno moja la kiarabu na madai dhidi yake kuwa alisaidia kundi la Brotherhood ni ya kushangaza sana.

Wamekuwa kizuizini tangu Disemba mwaka jana na mahakama kwa mara nyingine imewanyima dhamana.

Leo mahakama ilikuwa ichunguze ushahidi wa video, lakini hilo halikufanyika kwa sababu vifaa hivyo havikupatikana

Kesi yao imeahirishwa hadi tarehe 10 Aprili.

No comments: