Monday 5 December 2016

Mchezaji wa Mbao Fc U 20 afia uwanjani




Mshambuliaji wa timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20 wa Mbao Fc Ismail Mrisho Khalifani alifariki dunia jana jion katika mechi kati ya timu yake na Mwadui Fc iliyokuwa ikipigwa katika uwanja wa kaitaba mjini Bukoba ikiwa ni mchezo wa mwisho wa kumaliza mzunguko wa kwanza.
Kifo cha mshambuliaji Khalfani kilitokea baada ya kugongana na beki wa Mwadui Fc wakati akiwania mpira , Khalifani alifanikiwa kuamka na kuanguka tena , kutokana nan a kukosekana na gari la huduma ya kwanza Khalifan alibebwa na gari la zima moto katika juhudi za kutaka kuokoa maisha ya marehemu lakini kabla hajafikishwa hosipitali alipoteza maisha.
Ismail Khalfan kabla umauti kumfikia katika mechi hiyo alifanikiwa kuipatia timu yake goli la pili kupitia adhabu ya mkwaju wa penati ambayo hadi mwisho wa mchezo Mbao Fc 2- 0 Mwadui Fc

No comments: