Monday 5 December 2016

Waziri Mkuu afanya ziara ya Kushtukiza katika hosptali ya Mout Meru Arusha


Waziri Mkuu majaliwa akiwafariji wazazi walioko katika wodi ya wazazi katika hosipital ya Mout Meru

Waziri mkuu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania jana katika hali ya kushangaza alifanya ziara ya kushtukiza katika hospitali ya mkoa Mout Meru iliyoko mkoani Arusha. Ikumbukwe kuwa waziri mkuu yuko Arusha kwa ziara za kikazi.
Katika ziara hiyo ilitokana na malalamishi kutoka kwa wananchi juzi katika mkutano wa hadhara katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid kwamba hosipitali hiyo ina matukio ya wizi wa watoto wanaozliwa katika hospitali hyo.

Hata hivyo jana kwatika ziara hiyo waziri mkuu alishuhudia wodi ya wajawazito kitanda kimoja kikilaza watu watatu , na kuagiza hospitali za pembezoni kuboreshwa ili kupunguza msongamano wa wangonjwa mout meru.
Majaliwa akielekea katika Wodi ya wazazi
Akizungumzia sakata la wizi wa watoto katika hospital hiyo alivitaka vyombo husika kufanya uchunguzi dhidi ya tuhuma hizo hii inatokana wiki kama mbili zilizopita mzazi walda Musa kutuhumu hospital hiyo kwa kumwibia mwanae baada ya kujifungua “ Nilikuja hapa hospitali tarehe 4/10 na kutoka 7/10 nilijifungua kwa njia ya upasuaji ndipo walipomchukua mwanangu kwa madai wanampeleka katika chumba cha joto, siku ya kwanza akaja Mume wangu na kwenda kumwona mwanangu , siku ya pili pia alienda kumwona na kumkuta mwanetu ni mzima wa afya , Lakin siku ya tatu wakati tunatoka tulipotoka mimi na Mume wangu tuienda kumchukua mtoto na kuambiwa mtoto alifariki na hatukupata hata fulsa ya kuona hata mwili wake”
Dk. Jackline Urio Mganga mkuu mfawidhi wa Hospitali hiyo alipotakiwa kujibu tuhuma hizo alisema kuwa mtoto huyo baada ya kuzaliwa alipoteza maisha na baadae mwili wake ulipelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali hiyo.

No comments: