Wednesday 29 April 2015

Barca yazidi kujikita kileleni baada ya kuichapa Getafe 6-0

Messi,Neymar,Suarez waichakaza vibaya Getafe
Vinara wa La Liga FC Barcelona Jana Usiku wameishindilia Getafe Bao 6-0 na kupanda kuwa mbele ya Timu ya Pili Real Madrid kwa Pointi 5.
Mabao ya Barca yalifungwa na mshambuliaji wao hatari Lionel Messi aliyefunga mara mbili huku, Luis Suarez nae akitupia kambani mabao mawili , Neymar na Xavi wakifunga bao moja moja.
Mabao hayo ya washambuliaji wa Barca, Messi, Suarez na Neymar yamewafikisha zaidi ya mabao 100, kwa Msimu huu.
Hii Leo, Real Madrid walioko nafasi ya pili watakua na kibarua cha kupetetana na Almeria Uwanjani Santiago Bernabeu.
Vita ya kuwania kiatu cha mfungaji bora kiko kwa Cristiano Ronaldo mwenye magoli 39 akifuatiwa na Messi mwenye mabao 38.

No comments: