Tuesday 28 April 2015

Dau la Eden Hazard latangazwa

Zinedine Zidane alimsifia Gareth Bale kwamba ni mchezaji wa tofauti sana, baada ya summer kufika mwaka 2013 akahamia Real Madrid. Sasa wasiwasi umetanda kwa Hazard kuwa na uwezekano wa kuhamia Real baada ya Zidane kumsifia hivyo hivyo Hazard akimfananisha kama Cristiano na Messi kwa sasa.
Jose Mourinho akijibu kuhusu maneno ya Zidane alisema kwamba kama Real inamtaka Hazard, yeye (Mourinho) angekua wa kwanza kujua.Lakini kama ni kweli wanamtaka nay eye hajui basi itawagharimu £100 million kwa kila mguu wa Hazard.Mourinho alisema naweza kumuuza kwa Pauni 100 milioni, ikichanganywa na staa mwingine wa dunia (mwenye thamani ya Pauni 100 milioni) kwa hiyo inakuwa Pauni 200 milioni. Mchezaji huyo raia wa Ubelgiji ameonyesha kiwango cha maana katika msimu huu na jana Jumapili alikuwa akiwania tuzo ya PFA.
Mourinho ambae leo ana mechi na Arsenal alisema kwamba haamini kama Real wanajaribu kum-sign Hazard kwasababu bado hawajamwambia. Uhusiano wake na rais wa timu na CEO hautoi nafasi ya kitu kama hicho kutoka nyumba ya mgongo wake. Lazima wangemwambia kwasababu wana aminiana kikamilifu.
Chochote kinaweza kutokea na Real Madrid kwenye kuweka mzigo mzito kumpata yule wamtakae, sio tatizo kubwa kwao. Tusubili tuone.

No comments: