Naseeb Abdul au Diamond Platinumz anasifika zaidi Tanzania kwa kipawa chake cha uimbaji
Diamond alijizolea tuzo tatu, ikiwemo ya mwanamuziki mgeni mwenye kipawa kikubwa, mwanamuziki bora zaidi kwenye mtindo wa Afro-Pop na tuzo ya mwanamziki bora zaidi katika kanda ya Afrika Mashariki.
Hii ni mara ya pili mwaka huu kwa Diamond ambaye mwezi Mei alishinda tuzo saba katika mashindano mangine ya wanamuziki ikiwemo mwanamuziki bora zaidi wa kiume , mwandishi na mtunzi bora zaidi wa nyimbo pamoja na mtumbuizaji bora zaidi Tanzania.
Mwanamuziki Tiwatope Savaga wa Nigeria naye alijinyakulia tuzo ya mwanamuziki bora zaidi wa kike hasa kwa vile alivyoimba kibao chake 'Eminado'.
Tuzo hizo huandaliwa na kituo cha televisheni ambacho hucheza tu muziki cha Channel O.
No comments:
Post a Comment