Friday 19 December 2014

Mahakama nchini Uingereza yamnyima haki ya kufanya tendo la ndoa na Mkewe



Mahakama nchini Uingereza imemzuia mwanamume mmoja kufanya tendo la ndoa na mke wake ambaye ana matatizo ya kiakili kwa sababu hana uwezo wa kutoa ruhusa kwa mumewe.

Mwanamke huyo mwenye urmri wa miaka 39 ana ugonjwa wa kiakili wa kiwango cha nne na saba na ni mke mwenza wa mwanamke wa mke wa kwanza wa mumewe.

Mama huyo ana watoto wanne na kwa sasa na yuko chini ya uangalizi wa kituo cha afya kinachowashughulikia wagonjwa wenye matatizo ya akili.

Lakini jaji aliambiwa aamue iwapo anaweza kurejea kwa mumewe wa miaka 18 ambaye anataka kumwangalia katika nyumba yao ya mjini London.

Mume huyo anayejulikana kama SA alihoji kwamba ni haki yake kufanya tendo la ngono na wakeze,iwapo wana akili timamu ya kuweza kukubali na kwamba ni jukumu lao kukubali.

Alitaka mwanamke huyo kurudi nyumbani ili aweze kutekeleza tendo la ngono na wake zake wawili kwa siku tofauti.

Lakini Jaji Justice Mostyn ambaye alisema kuwa ndoa ya wake wengi chini ya sheria ya kiislamu ni halali lakini ni haramu nchini Uingereza aliamuru kwamba mwanamke huyo aliyetajwa kwa jina TB hana akili timamu ya kufanya uamuzi wa kutenda tendo la ngono,na kwamba si vyema yeye kurudi nyumbani.
Wana ndoa


Alisema:''Ushahidi unaonyesha wazi kwamba TB hajui tishio la kiafya linalomkabili.Alishindwa kulinganisha uja uzito na tendo la ngono.Mwathiriwa hajui vile watoto wake waliovyoingia katika tumbo lake kama anavyoeleza.Ijapokuwa alifurahia tendo la ngono hakujua kwamba alikuwa na haki ya kuchagua na kukataa. Kwa kweli tabia ya SA,kama ilivyo katika utamaduni na dini yake ni kwamba ana haki ya kutaka kufanya tendo la ngono na wakeze na kwamba wanawake hao wana jukumu la kukubali''.

Jaji huyo amesema kuwa juhudi za kumuhamasisha TB kuhusu tendo la ngono ,haki zake na hatari iliopo zimefeli.

Aliongezea kuwa TB licha ya kuwa amepata watoto wanne na mke huyo bado angepenbda kufanya tendo la ngono naye.

Maelezo ya hatua hiyo yamepatikana katika uamuzi uliondikwa na jaji huyo baada ya kusikilizwa katika mahakama ya utetezi ambayo inatathmini maswala kadhaa yanayohusiana na watu wagonjwa na wasioweza kujitetea.

Jaji Mostyn alikuwa ametakiwa kufanya uamuzi na shirika la London la Borough of Tower Hamlets linalosimamia maswala ya wanawake.

Mahakama iliambiwa kuwa wana ndoa hao walikuwa na uhusiano wenye utata na kwamba kulikuwa na wakati wa ghasia za kinyumbani wakati mume anapokuwa na hasira.

No comments: