Wednesday 31 December 2014

Ndoa za jinsia moja zaanza kufungwa huko uskochi

Joe na mwenzake Brown wakifunga ndoa nchini Uskochi

Harusi ya kwanza ya watu wa jinsia moja imefanyika huko Uskochi .
Joe Schofield na Malcom Brown walifunga ndoa katika sherehe iliofanyika katika eneo la Trade Hall Glasgow huku Susan na Gerrie Douglas -Scott wakifanya harusi yao katika eneo la faragha mjini humo.
Sheria hiyo mpya ya watu wa jinsia moja ilianza kufanya kazi Uskochi mapema mwezi huu.
Sherehe hizo zilihudhuriwa na waziri wa kwanza wa Uskochi.
Susan na mwenzake Gerrie wakifanya ndoa yao huko Uskochi
Nicola Sturgeon na mashirikishi wa chama cha Green Party Patrick Harvie MSP walishuhudia ndoa ya Susan na Gerrie naye mshairi wa kitaifa wa Uskochi Liz Lochhead na waziri wa serikali ya Uskochi Marco Biagi MSP wakihudhuria sherehe ya bwana Schofield na mwenzake bwana Brown.
Susan mwenye umi wa miaka 54 na Gerrie Douglas-Scott mwenye umri wa miaka 59 wanaishi mjini Galsgow ambapo walikutana miaka 18 na wana watoto wakubwa watano.
Walioana mwaka 2006 na kuamua kufanya sherehe mwaka huu.

No comments: