Monday 15 December 2014

Diamondi awakera wasanii wa Kenya

Diamond awakera wasanii wa KenyaMsanii maarufu wa Tanzania Diamond amewakera wasanii kutoka mji wa Mombasa akiwemo msanii mashuhuri Nyota Ndogo

Diamond ambaye aliwatumbuiza mashabiki wake katika tamasha lililoandaliwa mjini Mombasa aliwakera wasanii wenzake kutoka Mombasa akiwemo nyota wa pwani Nyota Ndogo.

Diamond anasemekana kumwomba mwandalizi wa tamasha hilo kuwaondoa wasanii wote waliokuwa katika sehemu ya VIP wakiwemo wasanii mashuhuri Susumila na Nyota Ndogo.

Wasanii mjini Mombasa waliungana kumkashifu Diamond na mwandalizi wa tamasha hilo huku DJ Delph akisusia kuhudumu katika tamasha hilo.

Wasanii hao walisema kuwa lilikuwa jambo la kusikitisha kuona kuwa wasanii kutoka pwani ya Kenya walibaguliwa wakiwa nyumbani.

No comments: