Tuesday 27 January 2015

Chelsea na Liverpool kumenyana leo Kombe la FA

Baada ya kushindwa kutambiana katika mchezo wa kwanza wa Kombe la FA uliomalizika kwa Sare ya 1-1 Chelsea na Liverpool watakuwa dimbani Stamford Bridge  kupimana ubavu.
Mchezo huu wa nusu fainali ya pili utaamua nani anaelekea fainali itakayopigwa katika dimba la Wembley Machi Mosi.
Katika mchezo wa kwanza Chelsea walipata goli kwa mkwaju wa penati kupitia kwa Eden Hazard huku Raheem Sterling akiisawaizishia Liverpool.
Mchezo mwingine wa nusu fainali ya pili utapigwa kati ya Sheffield United na Tottenham.
Tottenham walipata ushindi katika mchezo wa kwanza kwa bao 1-0 lilikwamishwa wavuni na Andros Townsend kwa mkwaju wa penati.

No comments: