Monday 12 January 2015

Mchezaji bora duniani kutangazwa

Tuzo ya mchezaji Bora wa dunia wa Fifa kwa mwaka 2014 inatarajiwa kutangazwa leo ambapo tayari wachezaji watatu wamechujwa ili kuania tuzo hiyo inayojulikana kwa jina la FIFA Ballon d'Or 2014.
Lionel Messi na Cristiano Ronaldo
Manuel Neuer
Wachezaji watatu waliobaki kwenye fainali ni pamoja na Christiano Ronaldo ambaye ni mchezaji wa timu ya Real Madrid na timu ya taifa ya Ureno.
Mwingine ni Lionel Messi mshambuliaji wa Barcelona na mchezaji wa timu ya taifa ya Argentina.
Na wa tatu ni Manuel Neuer Mlinda mlango wa Bayern Munich ambaye pia hudakia timu yake ya taifa ya Ujerumani

No comments: