Saturday 10 January 2015

Muhubiri wa kiislamu ahukumiwa kifungo cha maisha New York

Muhubiri wa kiislamu Abu Hamza aliyepewa kifungo cha maisha

Mhubiri wa kiislamu Abu Hamza amehukumiwa kifungo cha maisha gerezani kwa makosa ya ugaidi katika mahakama moja mjini New York.
Mhubiri huyo alifukuzwa nchini Uingereza mwaka 2012 kufuatia kesi ya muda mrefu na alipatikana na hatia miezi minne iliyopita.
Alipatikana na hatia katika mashtaka kadhaa ikiwemo njama ya kuwateka nyara watu kutoka nchi za magharibi ikiwemo Yemen mwaka 1998 na majaribio ya kuanzisha kituo cha mafunzo ya ugaidi kwenye jimbo la Oregon nchini Marekani.
Jaji alisema kuwa Abu Hamza alikuwa amewachochea watu wengine kuwaua wale wasio waislamu kama jukumu la kidini na kusema kuwa alikuwa hatari kwa jamii.
Alifahamika kwa kutoa hotuba kali kwenye msikiti mmoja mjini London.

No comments: