Monday 5 January 2015

Boko haramu yavamia kambi ya Jeshi


Boko Haram yaendelea kutekeleza mashambulizi yake nchini Nigeria
Kundi la Boko Haram lililoteka nyara vijana 40 kutoka mkoa wa Borno siku ya Jumamosi, sasa limevamia kambi ya jeshi la kimataifa iliyoko katika mji wa Baga.

Maafisa wakuu nchini Nigeria waliarifu kwamba kundi hilo lilibeba kila kitu kutoka kwenye kambi hiyo na kutoroka baada ya uvamizi.

Ndani ya kambi hiyo ya jeshi la kimataifa, mlikuwa na vikosi vya kijeshi kutoka Chad, Cameroon na Nigeria.

Baga ulikuwa ni mojawapo ya miji kadhaa ya mwisho iliyokuwa chini ya udhibti wa serikali. Jeshi la Nigeria limekuwa likiendelea kupambana na Boko Haram kwa miaka mitano katika mikoa mitatu ya kaskazini mwa nchi iliyokabiliwa na kundi hilo.

No comments: