Sunday 4 January 2015

Mwili wa shahid wa ICC wapatikana

Mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita ICC

Maafisa wa polisi nchini Kenya wameupata mwili wa shahidi muhimu wa mahakama ya ICC siku chache tu kabla ya kutoa ushahidi wake katika kesi ya naibu wa rais katika mahakama hiyo.
Ripoti za vyombo vya habari nchini Kenya zinasema kuwa mwili wa Meshash Yebei ulipatikana karibu na mto zaidi ya wiki moja baada ya kuonekana akibebwa na kuingizwa katika gari moja lisilo na nambari za usajili katika mji wa Eldoret,umbali wa kilomita 200.
Bwana Yebei alitarajiwa kusafiri kuelekea mjini Hague kwa kesi dhidi ya bwana Ruto-makamu wa rais ambaye anakabiliwa na mashtaka yanayohusiana na mashambulizi dhidi ya watu wa jamii ya kikuyu katika makaazi ya wakalenjin huko Rift valley wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi miaka saba iliopita.

No comments: