Thursday 8 January 2015

Meli Kubwa zaidi yatia nanga Uingereza kwa mara ya kwanza

Meli kubwa zaidi duniani imetia nanga nchini Uingereza kwa mara ya kwanza wakati huu ikiendelea na safari yake duniani, je Meli hii ina nguvu kiasi gani na ukubwa gani?
Meli iitwayo the Globe ina urefu wa mita 400 ikifananishwa na ukubwa wa mabwawa manane yanayotumika katika michuano ya Olimpiki ina upana wa mita 56.8 na upana wa mita 73 kwenda juu, ina uwezo wa kubeba mzigo wa tani 186,000.
Meli kubwa
 
Shuhuda wa Meli hiyo anasema ''ukiitazama meli hiyo utajihisi mbilikimo ni Meli kubwa mno''.
Safari ya Meli hiyo ilianzia mjini Qingdao nchini China tarehe 3 mwezi Desemba mwaka jana na inatarajiwa kumaliza ziara yake tarehe 25 Februari.
Hii ni meli ya kwanza kubwa zaidi kati ya meli kubwa tano zenye umbile kama Globe kutengenezwa Korea kusini, Meli zote zinatarajiwa kutolewa ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.

No comments: