Sunday 9 February 2014

AY; Diamond ni mtoto mdogo kwangu

NYOTA wa muziki wa Bongo fleva nchini, Ambwene Yesaya ‘AY’, amesema msanii mwenzake, Naseeb Abdul ‘Diamond Platinum’, hawezi kuathiri muziki wake kwani kila mtu ana malengo yake katika fani hiyo.

AY alitoa kauli hiyo kutokana na hisia za wadau wa muziki huo kwamba kung’ara kwa Diamond katika muziki huo, kunaweza kumfunika.

Kupitia mtandao wa Bongo5, AY alisema kila msanii ana mashabiki wake, hivyo hawezi kuhofia uwepo wa Diamond katika tasnia hiyo zaidi anampongeza na kumtakia mafanikio.

“Kila mtu ana malengo na mikakati yake katika kuyafikia mafanikio, hivyo sipo kwa ajili ya kujilinganisha na wengine, ushindani wangu ni dhidi ya yule anayetaka kutengeneza mkwanja mkubwa zaidi yangu,” alisema.

Msanii huyo ni kati ya wasanii ambao wanafanya vizuri kimataifa kutokana na kazi zao kukubalika na kuwavutia mashabiki wa muziki huo hapa nchini.

No comments: