Monday 24 February 2014

Hali yaendelea kuwa mbaya Africa ya kati

KUNDI la wanamgambo lenye nguvu kubwa huko Jamhuri ya Afrika Kati limesema litasalimisha silaha zake ikiwa tu, mahasimu wao wakuu wa kundi la Seleka linaloundwa na wapiganaji wengi wa Kiislamu litaweka silaha zao chini.
Kwa mujibu wa DW, kauli hiyo inaliweka taifa hilo katika muendelezo wa mgogoro nchini humo huku kundi la wapiganaji la anti-balaka lililoundwa mwaka jana likiwa na shabaha ya kuilinda jamii ya Kikristo ambayo imekuwa ikilengwa na waasi wa Seleka waliomuondoa madarakani rais wa taifa hilo mwezi Machi.
Tangu wakati huo kumekuwa na mauaji ya kulipiziana visasi licha ya kuwepo kwa maelfu ya wanajeshi wa kulinda amani wa kigeni nchini humo.
Msemaji wa anti-balaka, Sebastien Wenezou amesema wataweka silaha zao chini kwa masharti kwamba kundi la Seleka kuanza kufanya hivyo kwanza huku Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Kimoon akionya kutokea mauaji ya kuangamiza jamii kwa misingi ya kidini.

No comments: