Tuesday 18 February 2014

Kesi ya Lulu yaanza kunguruma

MSANII wafilamu nchini, Elizabeth Michael 'Lulu' ambaye anakabiliwa na kesi ya kumuua bila kukusudia msanii mwenzake, Steven Kanumba, amekiri kuwa alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na msanii huyo na kwamba walikuwa na ugomvi.
Lulu alikiri hayo jana wakati akisomewa mashtaka yake mbele ya Jaji Rose Temba wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam ambapo Lulu baada ya kusomewa mashtaka alikana.
Mbali na kukiri kuwa na uhusiano, pia Lulu alikiri kuwa baada ya tukio alitoka nje ya chumba walichokuwepo na kwenda kumwambia mdogo wake marehemu Kanumba, Setti Bosco kuwa marehemu amedondoka.
Akisoma hati ya mashtaka Wakili Mwandamizi wa Serikali, Monica Mbogo, alidai kuwa Aprili 7, mwaka 2012, Sinza Vatikani, Dar es Salaam, mshtakiwa alimuua bila kukusudia msanii Kanumba .
Wakili Kombo, alidai kuwa pamoja na mambo mengine, marehemu Kanumba baada ya kufa, mwili wake ulipelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo majibu yalionesha kwamba kifo chake kilisababishwa na uvimbe ndani ya ubongo.
Upande wa serikali una mashahidi watano pamoja na vielelezo wakati upande wa utetezi unatarajia kuwa na mashahidi watano na vielelezo.

No comments: