Tuesday 11 February 2014

Namweshimu sana Jaquar

Mwanamuziki Vivian Wambui, amewaomba wapenzi wa muziki kumheshimu na kuacha kumuhusisha na tuhuma za uhusiano wa kimapenzi na Jaguar.

Amesema anaweza kuwa na uhusiano na mtu yeyote anayempenda lakini siyo kwa watu anaowaheshimu kama Jaguar.

“Naomba mniheshimu, Jaguar ni kama kaka yangu jinsi tunavyoheshimiana na anavyonishauri kwa nia njema, sioni sababu ya kila kukicha kusema ni mpenzi wangu mnanidhalilisha,” alisema Vivian, alipohojiwa kwa njia ya simu na mtandao wa Bigeye.

Vivian alifafanua kuwa jambo la maana kwao ni kutathmini muziki wanaokufanya badala ya kuanzisha maneno ya ajabu ambayo yanaishushia hadhi tasnia ya muziki, kwa kuonekana ni kama kituo au kazi ya kuendeshea uhuni.

No comments: