Wednesday 12 February 2014

Chelsea yatoka sare ya 1-1 na West Brom

Chelsea imepoteza nafasi ya kuhakikisha kuwa imesalia kileleni mwa ligi kuu ya Premier ya Uingereza, mbele ya mahasimu wao Arsenal, baada ya kutoka sare ya kufungana bao moja kwa moja na West Brom, katika mechi iliyochezewa katika uwanja wa Hawthorns.

Victor Anichebe aliifungia West Brom bao hilo muhimu kunako dakika ya 87 Na kuinyima Chelsea alama mbili ambazo zingeihakikishia Chelsea hakikisho la uongozi wa ligi hiyo hadi juma lijalo.

Branislav Ivanovic aliiweka Chelsea mbele dakika ya 45, bao ambalo lilikuwa limeipa vijana hao wa Jose Mourinho kuwa alama nne mbele ya Arsenal ambayo kwa sasa inashikilia nafasi ya pili.

Arsenal imeratibiwa kucheza na Manchester United, siku ya Jumatano usiku na ikiwa Arsenal itashinda mechi hiyo itajihakikisha nafasi ya kwanza kwenye msururu wa ligi hiyo inayokwenda mapunzikoni mwishoni mwa juma hili ili kuruhusu mechi za kuwania kombe la FA.
Wachezaji wa Arsenal

Matokeo zaidi

Katika matokeo mengine ya mechi za ligi kuu zilizochezwa hiyo jana, Southampton iliilaza Hull City bao moja kwa bila.

Mlinda lango wa Southampton, Jose Fonte ndiye aliye bahatika kufunga bao hilo kufuatia purukushani katika lango la Hull City.

Dakika chache baada ya kufunga bao hilo, Fonte alivurumisha kombora kali ambalo liliokolewa na kipa wa Hull Jay Rodriguez.
Kocha Sam Allardyce

West Ham imepanda hadi nafasi ya kumi kwenye jadwali ya ligi hiyo baada ya kuilaza Norwich kwa magoli mawili kwa bila.

Ushindi huo ulikuwa wa tatu mfululizo kwa timu hiyo iliyo na makao yake Mashariki mwa jiji la London.

Norwich kwa upande wake inashikilia nafasi ya kumi na sita alama moja mbele ya West Brom na Sunderland iiliyo katika nafasi ya kumi na saba na kumi na nane mtawalia.

Cardif nayo imesalia katika nafasi ya mkia baada ya kutoka sare ya kutofungana bao lolote na Aston Villa.

No comments: