Friday 14 February 2014

Liverpool, Tottenham 'ngoma inogile'

NAHODHA wa Liverpool, Steve Gerrard juzi usiku aliifungia timu yake bao kwa mkwaju wa penalti dakika za majeruhi na kuisaidia klabu yake kuilaza Fulham mabao 3-2. Bao la kujifunga la beki Kolo Toure, liliipa Fulham uongozi kabla y a Daniel Sturridge kusawazisha.
Lakini kadri mechi hiyo ilipoendelea Fulham , walionesha mchezo mzuri na kuongeza bao la pili kupitia k w a Kieran Richardson, baada ya kipa wa Liverpool, Martin Skrtel kufanya masihara kwenye eneo la hatari.
Uongozi huo wa mabao 2 wa Fulham, hata hivyo haukudumu baada ya Phillippe Coutinho kuisawazishia Liverpool.
Timu hizo mbili zilionekana kugawana pointi moja kila mmoja lakini Liverpool, ilibahatika pale Sascha Riether alipomfanyia madhambi Sturridge katika dakika za ziada.
Nahodha wa Liverpool Gerrard, hakufanya makosa baada ya kukwamisha mkwaju wa penalti na kuandika bao la tatu na kuifanya timu yake kuwa na pointi nne nyuma ya vinara wa ligi hiyo Chelsea.
Ushindi huo ulikuwa wa tano kwa Liverpool, mwaka huu na hii inamaanisha kuwa vijana hao wa Brendan Roggers, wana nafasi ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu mwaka huu na pia kudumisha rekodi ya kutoshindwa mechi yoyote mwaka huu.
Katika mechi nyingine, Emmanuel Adebayor kwa mara nyingine alifunga mabao mawili na kudumisha harakati za Tottenham za kusalia katika nafasi nne bora kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza.
Tottenham waliilaza Necastle kwa mabao 4-0 katika mechi ya ligi hiyo iliyochezwa juzi usiku.
Adebayor alifunga bao la kwanza dakika ya 19 baada ya kipa wa Newcastle, Tim Krul kutema mkwaju uliopigwa na Nabil Bentaleb.
Mshambuliaji huyo raia wa Togo, vilevile alichangia bao la pili wakati kipa Krul kwa mara nyingine alipoutema mkwaju wake na kuumpa nafasi, Paulinho kumalizia na kufunga la pili.
Nacer Chadli aliifungia Totenham bao la tatu, baada ya kupiga kombora kali akiwa umbali wa mita 20.
Juhudi za Newcastle ziliishia ukingoni pale kipa wa Totenham, Hugo Lloris alipookoa mikwaju iliyopigwa na Papiss Cisse, Mathieu Debuchy na Yoan Gouffran.
Newcastle sasa haijafunga bao lolote katika mechi saba kati ya nane zilizopita na pia kuandikisha rekodi ya kupoteza mechi nne mfululizo katika uwanja wao wa nyumbani kwa mara ya kwanza tangu mwaka wa 1987.
Nayo Arsenal imepoteza nafasi ya kurejea tena kileleni mwa ligi hiyo, baada ya kutoka suluhu na Manchester United katika uwanja wao wa nyumbani wa Emirates.
Vijana hao wa Arsene Wenger, walikuwa wakijaribu kufuta aibu waliyoipata wiki iliyopita wakati walipofungwa mabao 5-1 na Liverpoool nayo Manchester United, kwa upande wake ilikuwa ikijinasua baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 na Fulham mwishoni mwa juma lililopita.

No comments: