Wednesday 30 April 2014

Chelsea uso kwa uso na Atletical Madrid

mpinzani-wa-real-madrid-kubainikaTimu ya pili itakayochuana katika fainali ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya itabainika leo Chelsea watakapochuana na Atletico Madrid.

Awamu ya pili ya nusu fainali itasakatwa katika uga wa Stamford Bridge saa 21:45 saa za Afrika Mashariki.
Wasiwasi wa Chelsea
Timu ya Chelsea itakosa huduma za wachezaji muhimu kutokana na majeraha na adhabu ya kutocheza mechi ya leo. Petr Cech aliyepata jeraha la bega na John Terry watakosa mechi ya leo kutokana na majeraha huku John Obi Mikel na Frank Lampard wakikosa idhini ya kucheza kutokana na adhabu ya kati ya Manjano. Mohamed Salah na Nemanja Matic hawakujumuishwa katika orodha ya wachezeja na hivyo basi hawataweza kuvalia jezi usiku huu.
Je Atletico wataandika historia mpya?
Atletico Madrid inatazamia kuandika historia mpya ya kufika katika fainali ya ligi ya Mabingwa kwa mara ya kwanza. atletico watamkosa mchezaji wao machachari ambaye alionyeshwa kadi ya manjano ya pili katika awamu ya kwanza. Arda Turan hatarajiwi kuwa katika timu itakayoanza kutokana na majeraha.
Je Diego Simeone atafanikisha ndoto ya Atletico au Mourinho ataonyesha ubabe wake?

No comments: