Wednesday 30 April 2014

Bunge la Libya lashambuliwa

bunge-la-libya-lashambuliwaUchaguzi wa serikali ya muda uliokuwa ukifanyika katika bunge la Libya wakatizwa.

Uchaguzi wa serikali ya muda uliokuwa ukifanyika katika bunge la Libya wakatizwa.
Watu wasiotambulika walitekeleza mashambulizi ya silaha katika bunge la Libya na kukatiza uchaguzi huo.
Washambuliaji waliingia katika uwanja wa bunge uchaguzi ulipokuwa ukiendelea na kuanza kufyatua risasi na kuwajeruhi watu kadhaa.
Awamu ya kwanza ya uchaguzi ilimalizika huku ya pili ikiahirishwa hadi siku iliyofuata.
Waziri mkuu wa Libya Abdullah El Tani alijiuzulu baada ya kulengwa katika mashumbulizi hayo.
Katika tukio jingine, hakimu wa zamani Ahmad Bu Acile el-Mansuri alivamia na kuuawa katika mji wa Derane lililoko katika jimbo la el-Kubbe Mashariki mwa nchi hiyo. Mansuri alihudumu katika mahakama kuu kabla ya mapinduzi yaliyotekelezwa tarehe 17 mwezi Fubruari. Kufikia sasa hakuna taarifa rasmi iliyotolewa kuhusiana na mauaji hayo

No comments: