Sunday 13 April 2014

Nigeria ya dai Mugabe ameitusi

Mwanabalozi wa Zimbabwe nchini Nigeria ameitwa akajieleze kwa sababu ya matamshi ya Rais Robert Mugabe kuhusu rushwa.

Mwezi uliopita Rais Mugabe alilalamika kuwa Wa-Zimbabwe wanaanza kuwa kama Wa-Nigeria - wakitaka jambo lifanyike inabidi watie mkono mfukoni.

Wizara ya mashauri ya nchi za nje ya Nigeria imemwambia balozi wa Zimbabwe, Stanley Kunjeku, kwamba hawakubali shambulio hilo la kuwatusi.

No comments: