Tuesday 29 April 2014

Mama awaua wanawe 3 walemavu


Baba ya watoto hawa alikuwa safarini nchini Afrika Kusini wakati mauaji yalipofanyika.
Mama anayetuhumiwa kwa mauaji ya watoto wake watatu nchini Uingereza amewekwa rumande kwa ukaguzi wa kiakili kubaini ikiwa alikuwa timamu wakati wa mauaji hayo.
Tania Clarence, mwenye umri wa miaka 42, alihudhuria kikao cha mahakama kwa njia ya video akiwa gerezani akituhumiwa kwa mauaji mapacha wake wawili wenye umri wa miaka mitatu na mwanawe msichana mwenye mwiri wa miaka minne.
Watoto hao walemavu, walipatikana nyumbani kwao katika mtaa wa New Malden wakiwa wamefariki Aprili 22.
Mahakama pia ilisikia kuwa watoto hao walikuwa na ulemavu uliosababishwa na ugonjwa wa uti wa mgongo.
Mahakama iliambiwa kuwa watoto hao walifariki katika hali ya kuzuiwa kupumua.
Jaji Judge Brian Barker, alisema Bi Clarence anaweza kuondolewa jela na kuwekwa rumande kufanyiwa uchunguzi na kupokea matibabu ya kiakili kwa sababu tukio hilo sio la kawaida
''Hio sio dhamana , lakini ninachoamrisha ni aweze kufanyiwa ukaguzi wa kiakili kuambatana na kifungu cha 35 cha sheria. Baada ya hapo anaweza kuwekwa rumande ili achunguzwe zaidi hali yake, '' alisema jaji.
Wendesha mashitaka waliambia mahakama kuwa polisi walikuwa wanasubiri matokeo ya uchunguzi wa maiti za watoto kabla ya kubaini chanzo cha vifo vyao.
Mahakama iliambiwa kuwa babake watoto hao alikuwa nchini Afrika Kusini na mwanao mkubwa wakati wa mauaji hayo.
Mahakama itasikia baadaye utetezi wa Bi clarrence ikiwa anakiri au kukana mauaji tarehe 15 mwezi ujao.

No comments: