Tuesday 29 April 2014

Wanajeshi wa Israel wabomoa msikiti

Wanajeshi wa Israel walivunja msikiti mmoja na nyumba 4 za wapalestine mjini Nablus.

wanajeshi-wa-israel-wabomoa-msikitiKulingana na taarifa iliyotolewa na mwanachama wa Kamati ya Upinzani cha Umma wa Palestine, Yusuf Deyriyye, Wanajeshi wa Israeli walivamia na kubomoa msikiti huo uliojengwa miaka sita iliyopita na nyumba nne huku wakidai kuwa zilikuwa zimejengwa bila idhini.
Deyriyye alisema kuwa wanajeshi wa Israel walikua wametoa onyo kuhusiana na msikiti huo na nyumba hizo. Aliongezea kusema kua " kwa miaka mingi Israel imekuwa ikitumia kisingizio hicho kuharibu nyumba za Wapalestine."
Israel bado haijatoa taarifa rasmi kuhusiana na shambulizi hilo.
Mashambulizi kama haya yaliwahi kutendeka katika kijiji hicho cha Et-Tavil yenye wakaazi wanaojishughulisha na kilimo na ufugaji.

No comments: