Wednesday 30 April 2014

Maandamano dhidi ya serikali ya Nigeria

Maandamano kuhusu wasichana waliotekwa
Maandamano makubwa ya kwanza yanatarajiwa kufanyika katika mji mkuu wa Nigeria- Abuja baadaye leo watu wakiitaka serikali kuchukua hatua zaidi kuwanusuru wasichana 200 wa shule waliotekwa nyara na wanamgambo wa kiislam .
Wasichana hao walichukuliwa kutoka shule yao ya malazi iliyopo katika eneo lisiloweza kufikiwa kwa urahisi kaskazini mashariki mwa nchi zaidi ya wiki mbili zilizopita.
Waandalizi wa maandamano hayo wanaita serikali kuelekeza juhudi zao kwa wasichana waliopotea .
Mpango ni kuandamana hadi bungeni na kwa mshauri wa taifa wa masuala ya usalama na kuwasilisha barua ya kutoa wito wa kufanyika kwa juhudi zaidi kuwanusuru wasichana hao.
Mwanaharakati mmoja wa kijamii amesema katika nchi nyingine yoyote ile suala la kutekaji nyara wa wasichana hao wengi lingekuwa ni mjadala wa kila siku .
Lakini serikali ya Nigeria imekuwa ikikabiliwa na ukosoaji mkubwa kwa kukaa kimwa huku wazazi wenye shauku wakisailia kuwa gizani kuhusu nini kinachoendelea kuhusiana na wasichana wao.
Huenda kwa kuhisi hilo rais wa Seneti , David Mark, sasa amezungumza. Amewatolea wito watekaji kuawaachilia mara moja wasichana bila masharti na akasema bila shaka taifa letu liko vitani .

No comments: