Sunday 27 April 2014

JB afungua kasino Babu kubwa

KAKA mkubwa anayeongoza kwa mvuto kwenye sinema, Steven Jacob ‘JB’ ndiye msanii pekee kati ya wasanii wa filamu za Kibongo aliyealikwa kwenye uzinduzi wa Casino kubwa la kisasa la Princess lililopo katikati ya Jiji la Dar es Salaam.
JB alialikwa na wageni wengine maarufu akiwemo Balozi wa Uturuki nchini, Ali Davutoglu aliitumia fursa hiyo kutanua mtandao wa kufahamiana na watu wengi mashuhuri.
Balozi Davutoglu alisema Casino hiyo ni sehemu muhimu kwa wasanii, wanamuziki na watu wanaopenda sanaa na utamaduni wa Tanzania na nchi nyingine kukutana na kubadilishana mawazo.
Naye JB aliliambia gazeti hili kwamba amefurahia mwaliko huo na kuongeza kuwa sehemu hiyo ni muhimu sana kwa wasanii wa filamu, wanamuziki na watu wengine kujumuika pamoja na kupata uzoefu wa kimataifa.

No comments: