Thursday 27 November 2014

Aliyekuwa kocha wa Chelsea kuinoa Ghana

Mkufunzi wa zamani wa Chelsea Avram Grant ameteuliwa kuwa kocha mpya wa Ghana.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 59 alitia saini kandarasi ya kufunza kwa miezi 27 na kuchukua uongozi kutoka kwa Maxwell Konadu, ambaye amekuwa kocha wa muda tangu Kwesi Appiah alipoondoka mwezi wa Septemba.
Ataanza kazi Jumatatu na mkataba wake kumalizika mwishoni mwa Februari 2017 - baada ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika.
Avram Grant alipokuwa mkufunzi wa timu ya Chelsea.
Raia huyo wa Israeli ana wiki sita tu kuiandaa Black Stars kwa ajili ya kombe la mataifa ya Afrika mwaka 2015 nchini Equatorial Guinea.
Shirikisho la kandanda nchini Ghana limetoa ruzuku kwake kwa "kufanya vizuri" katika mashindano hayo na amepewa muda mfupi na timu hiyo na kuwa atashinda kombe hilo miaka miwili ijayo.
Ghana, ambayo iliongoza katika kufuzu kwenye kundi lao ili kushiriki mashindana hayo mwaka ujao, itapata kujua wapinzani wao nchini Equatorial Guinea wakati droo itakapofanywa tarehe 3 Desemba.
Mashindano yatafanyika kati ya Januari 17 na 8 Februari.
Grant, ambaye alikuwa kocha mkuu wa timu ya Chelsea alishindwa na Manchester United katika fainali za mwaka wa 2008 katika Ligi ya Mabingwa, alipohudumu hadi hivi majuzi ambapo alichaguliwa kuwa mkurugenzi wa kiufundi katika klabu ya BEC Tero Sasana nchini Tahailand.
Jukumu lake la mwisho kama kocha lilikuwa katika klabu ya Partizan Belgrade kati ya mwaka 2012-2014, wakati ambapo aliongoza klabu hio kutwaa ubingwa wa ligi kwa mara ya tano.
Timu ya soka ya Ghana
Kando ya kuviongoza vilabu vya Uingereza vya Portsmouth na West Ham, Grant ana uzoefu wa kimataifa kwani aliifunza timu ya taifa ya Israeli kwa miaka minne.
Kumekuwa na wale wamekuwa na wasiwasi kwamba utaifa wa Grant ungeweza kumzuia kuingia baadhi ya nchi za Afrika Kaskazini.
Rais wa shirikisho la kandanda nchini Ghana, Kwesi Nyantekyie aliiambia BBC Michezo "kwamba ni suala" lakini anasema kuwa pande hizo mbili zitakabiliana nalo.
"Mmiliki wa pasipoti ya nchi ya Israel hatakataliwa tu kuingia nchi za Afrika Kaskazini,bali pia atazuiliwa kuingia baadhi ya nchi za Kiarabu," alisema.
"Yeye ameleta njia mbadala ya kukabiliana nayo. Kuna utaratibu wa kuridhisha wa kukabiliana na tishio lake.
Hivi karibuni, katika miezi michache ijayo, tutashughulikia kikamilifu mambo hayo."

No comments: