Kauli ya Mbwezeleni imekuja baada ya katibu mkuu
wa TFF, Celestine Mwesigwa kusema kuwa tayari wamewasilisha suala hilo
la Ndumbaro kwenye kamati husika, lakini kamati hiyo ndiyo
inayochelewesha.
Akizungumza na gazeti hili kuhusu suala hilo,
Mbwezeleni alisema hakuna rufaa yoyote iliyowasilishwa kwenye kamati
yetu. Kwa kawaida rufaa ikikatwa, TFF wanatuandikia kutujulisha, lakini
hakuna chochote ambacho wameshatuambia mpaka sasa zaidi ya kusikia
kwenye vyombo vya habari.
“Ninavyoongea na wewe narudi zangu Zanzibar
nilikuja Bara mara moja, na sijaambiwa lolote mpaka muda huu. Hatuwezi
kukutana wakati TFF hawajaileta rufaa hiyo mezani mwetu.”
No comments:
Post a Comment