Tuesday 4 November 2014

Imebaki mechi moja tu simba kuvunja rekodi ya Man City na Norwich city

MATOKEO ya wikiendi iliyopita ya Ligi Kuu ya Vodacom yaliwaacha mashabiki wa soka katika mshangao. Iko hivi Ndanda FC waliichapa Azam FC bao 1-0. Simba wakatoa sare nyingine ya bao 1-1 na Mtibwa na Yanga ikapigwa bao 1-0 na Kagera Sugar.
Sababu kuu ya Simba ni kuingia katika rekodi ya kipekee hapa nchini baada ya kucheza mechi ya sita mfululizo ikipata matokeo ya sare. Jumamosi iliyopita ilitoshana nguvu na Mtibwa kwa sare ya 1-1.
Wana Msimbazi hao wana magoli sita ya kufunga na sita ya kufungwa,matokeo haya yamezidi kuwanyong’onyesha mashabiki wa Simba, mwanya uliotumiwa na wale wa Yanga kuficha aibu yao ya kipigo huko Kaitaba.
Wakati Wekundu wa Msimbazi wakijiuliza kwa yanaoendelea, Simba imejikuta ikiingia kwenye orodha ya timu zilizoambulia sare nyingi za mfululizo. Timu za Manchester City, Southampton na Norwich City kwa miaka tofauti zilijikuta katika historia ya miongoni mwa timu ambazo zilitoa sare nyingi za mfululizo katika Ligi Kuu England.
Timu hizo tatu za England ziliambulia sare saba katika misimu tofauti. Kumbukumbu zinaonyesha kuwa, Norwich City ilicheza michezo kati ya 38 hadi 42 katika msimu wa 1993-1994 na kujikuta ikipata sare saba mfululizo.
Msimu uliofuata, 1994-1995, Southampton nayo ilicheza idadi kama hiyo ya mechi na kujikuta ikiambulia sare saba mfululizo.
Kama hiyo haitoshi, Manchester City nao walijikuta katika orodha hiyo ya sare saba mfululizo katika msimu wa 2009-2010.
Manchester City pia wamo katika orodha ya timu zinazoongoza kwa kutoa sare nyingi kwa msimu mzima wa ligi kwani katika msimu wa 1993-1994 ilicheza mechi 42 jumla na kupata sare 18.
Simba inapaswa kushinda mechi inayofuata la Ligi Kuu Bara ili kukwepa kuzifikia timu hizo za England kwa idadi kubwa ya sare za mfululizo.

No comments: