Sunday 23 November 2014

Mancity na chelsea zaua, Arsenal ya lala dhid ya Man u

Chelsea striker Diego Costa chests the ball as the striker continued his dominance in the Premier League against West BromChelsea imeendelea kujiimarisha kileleni mwa Ligi Kuu England ikiwa na pointi 32 bila mpinzani baada ya kuilaza West Brom kwa mabao 2-0.
Nao, Manchester City waliilaza Swansea kwa mabao 2-1 katika mchezo mwingine wa ligi hiyo kwenye Uwanja wa Etihad.
Mabao ya Diego Costa na Eden Hazard, kipindi cha kwanza yaliiwezesha Chelsea kuibuka na ushindi dhidi ya West Brom iliyocheza muda mrefu na wachezaji 10 baada ya Claudio Yacob kutolewa kwa kadi nyekundu.
Swansea walitangulia kufunga bao kupitia kwa Wilfried Bony kabla ya Steven Jovtric kusawazisha na Yaya Toure kumaliza kazi, kipindi cha pili.
Kwingineko matokeo yalikuwa:Stevan Jovetic
Everton 2-1 West Ham, Newcastle 1-0 QPR, Stoke 1-2 Burnley, Leicester 0-0 Sunderland
Wakati huohuo, nahodha wa zamani wa Manchester United, Paul Ince anaamini kuwa klabu yake hiyo ya zamani haikutakiwa kumruhusu Danny Welbeck kuondoka.
Welbeck, ambaye sasa ana miaka 23, aliyekuwa Old Trafford akiwa na miaka minane, alijiunga na Arsenal kwa ada ya uhamisho ya Pauni 16 milioni.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa England alipangwa kuivaa timu yake ya zamani katika mchezo wa jana usiku wa Ligi Kuu England kwenye Uwanja wa Emirates.
“Alipoondoka Manchester United ilikuwa ni mshituko. Alikuwa na uwezo wa kucheza nyuma ya mshambuliaji wa mwisho na kutengeneza nafasi kwa wengine kufunga.

No comments: