Thursday 19 December 2013

MAMA SHARO BILIONEA AMLIZA RICH MAVOKO

STORI kuhusu maisha ya mama mzazi wa staa wa komedi Bongo, marehemu Husein Mkiety ‘Sharo Milionea’, baada ya kifo cha mwanaye huyo imemliza Rich Mavoko ambaye alikwenda kumtembelea nyumbani kwake kijijini Lusanga, Muheza mkoani Tanga.

Rich Mavoko akifuta machozi alipomtembelea Mama Sharo Milionea.

Akiteta machache na Risasi Vibes, Mavoko alisema, yeye kama msanii aliguswa kwenda kumsalimia mama Sharo kwa kuwa wote ni wasanii na aliona mama huyo anahitaji faraja kutoka kwa watu waliokuwa karibu na mwanaye.

“Mama alifurahi sana kuniona. Tulizungumza mengi lakini niliguswa sana na matatizo aliyonayo mama yetu. Mama anasema, mali nyingi za marehemu mwanaye, amekuwa akizisikia tu lakini hajapewa.

Mavoko na Mama Sharo wakiwa katika kaburi la Marehemu Sharo Milionea.

“Kiukweli mama Sharo anatia huruma sana kwani faraja imepotea, mali za mwanaye hazioni, amebaki akitia huruma.
Unajua marehemu alikuwa akimsadia sana mama yake, ndiyo lilikuwa tegemeo lake kubwa. Ameondoka na kumuacha akiwa hana la kufanya, mbaya zaidi hata mali zake ambazo zingepaswa kumsaidia kipindi hiki, wajanja wamezidhulumu.

“Dunia haina usawa kabisa. Kiukweli inatia huruma sana. Nawasihi wasanii wenzangu na wadau wa sanaa, inatakiwa tukumbuke wenzetu waliotangulia tena kwa kuwaenzi kwa kila njia.

Marehemu Sharo Milionea enzi za uhai wake.

Kuna vitu vinauma sana amenieleza tangu kifo cha mwanaye haki zake nyingi hajui zilipo. Tuungane wasanii tuwasaidie wazazi wa wasanii wanaotangulia mbele za haki,” alisema Mavoko.

No comments: