Sunday 8 December 2013

TB yaratibu na kuongoza msafara wa kuupanda mlima Kilimanjaro


Picture
Mwenyekiti wa TTB Balozi Sanga (wa pili kushoto)sambamba na wapanda mlima expedition wakichanja mbuga kuelekea kituo cha Mandara.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania – TTB anaongoza timu ya watu saba miongoni mwao wakiwemo wafanyakazi wa Bodi ya Utalii Tanzania kupanda mlima Kilimanjaro ambao pia ni mrefu kuliko yote barani Afrika na ambao pia ni miongoni mwa maajabu saba ya asili barani Afrika.

Msafara huu ujulikanao kama Uhuru Expedition  ambao ni mahsusi kwa ajili ya kuadhimisha miaka 52 ya uhuru umeratibiwa na kufadhiliwa na Bodi ya Utalii Tanzania umeanza kupanda mlima Kilimanjaro tarehe 6/12/2013 umeanza kupanda mlima Kilimanjaro tarehe 6/12/2013 umeanza kupanda mlima Kilimanjaro tarehe 6/12/2013 kupitia njia ya Marangu na unatarajia
Picture
Msafara wa Uhuru expedition katika picha ya pamoja na waongoza wapamda mlima muda mfupi kabla ya kuanza kupanda mlima Kilimanjaro kupitia njia ya Marangu.
Kumaliza zoezi hilo tarehe 10/12/2013.

Msafara huo wenye jumla ya wapandaji mlima saba (7) ambapo kutoka TTB ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Balozi Charles Sanga, Bw. Musa Kopwe na Bw. Hillary Mushi. Aidha katika msafara huo yumo pia Meja Jenerali mstaafu Gimonge, Bley Mayo, Bibi Lidya Kayuni na Bw. Joan Mwamlima wote kutoka Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Hii ni mara ya pili kwa Bodi ya Utalii Tanzania kuratibu msafara huu kwa lengo la kuadhimisha siku ya uhuru wa Tanzania Bara. Mara ya kwanza kwa TTB  kufadhili Uhuru Expedtion ilikuwa ni mwaka jana ambapo pamoja na TTB Kampuni nyingine kama ya  bia ya Serengeti ilijitoleza pia kudhamini Msafara huo wa Uhuru ulioongozwa  na aliyekuwa mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Jenerali mstaafu George Waitara.
Picture
Mkuu wa kitengo cha utalii cha Hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro (KINAPA) Bw. Mombo akitoa maelezo kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TTB Balozi Charles Sanga (kushoto) na Meja Jenerali mstaafu Gimonge kuhusu njia mbalimbali zinazotumika katika kupanda mlima Kilimanjaro muda mfupi kabla ya Balozi Sanga kuanza kuongoza msafara wa kupanda mlima.

No comments: