Thursday 10 July 2014

Rais wa China akutana na Rais wa Ethiopia


Rais Xi Jinping wa China amekutana na rais Mulatu Teshome wa Ethiopia katika jumba la mikutano ya umma mjini Beijing. Kwenye mkutano wao Rais Xi Jinping amesema China na Ethiopia zinaungana mikono na kusaidiana, na uhusiano kati ya nchi mbili ni mzuri, na ni mfano wa kuigwa kati ya China na nchi za Afrika, na kati ya nchi zinazoendelea. Amesema China inaungana mkono kithabiti na Ethiopia katika juhudi zake za kustawisha taifa, na inapenda kubadilishana uzoefu na Ethiopia kuhusu utawala na na kuimarisha ushirikiano katika pande mbalimbali.. Rais Mulatu amesema Ethiopia na China zinaelewana na kuaminiana kwa muda mrefu, serikali na wananchi wa Ethiopia wanaishukuru China kwa uungaji mkono na misaada inayotoa kwa miaka mingi. Sasa wakati Ethiopia inapohimiza maendeleo ya uchumi, inapenda kuiga uzoefu wa China. Pia amesema Ethiopia inaukaribisha uwekezaji wa China, na inapenda kupanua ushirikiano wa nchi hizo katika sekta za kilimo, utengenezaji na ujenzi wa miundombinu..

No comments: