Saturday 12 July 2014

Mwanasheria aliyefanya ukatili dhidi ya Msichana wake wakazi apelekwa rumande

http://freemedia.co.tz/daima/wp-content/uploads/2014/07/rwechengura_2.jpgMWANASHERIA Yastinter Rwechungura (44), mkazi wa Boko-Njiabanda, jijini Dar es Salaam, anayekabiliwa na kesi ya kumfanyia ukatili msichana wake wa kazi, Merina Mathayo, amerudishwa rumande bada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.
Masharti hayo ni kuwa na wadhamini wawili watakaosaini bondi yenye thamani ya sh milioni 4 kila mmoja, lakini alishindwa kuyakamilisha kwa kukosa mdhamini mmoja tu.
Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni, Amaria Mushi, alisema mshitakiwa huyo arudishwe rumande kwa kuwa ameshindwa kutimiza masharti  kutokana na kuwa na mdhamini mmoja. Kesi imeahirishwa hadi Julai 29, mwaka huu itakapotajwa tena.
Awali Mwendesha Mashitaka, Wakili wa Serikali, Masini Mussa, alidai mgonjwa ambaye ndie mlalamikaji, afya yake inaendelea vizuri, hivyo hapingi suala la dhamana kwa mtuhumiwa kwani ni haki yake kisheria.
Mshitakiwa huyo anadaiwa kutenda kosa hilo Juni 6 mwaka huu nyumbani kwake maeneo ya Boko-Njiapanda kwa kumpiga Merina kichwani kwa kutumia waya wa kompyuta na brenda, hali iliyomsababishia majeraha makubwa.

No comments: