Sunday 20 July 2014

Dogo Janja arudi tena Tip Top Connection

KINDA wa muziki wa kizazi kipya nchini, Abdulaziz Abubakari ‘Dogo Janja’ amerejea tena jijini Dar es Salaam katika kundi la Tip Top Connection baada ya kuwa mbali na kundi hilo kwa muda mrefu.
Dogo Janja arejea Tip Top Connection
Dogo Janja aliondoka katika Tip Top mwaka 2012 na kuhamishia kazi zake kwao Arusha baada ya kugombana na kiongozi wa kundi hilo, Ahmed Ally ‘Madee’ aliyeonekana kama mbaya hadi kuamua kujiweka mbali na msanii huyo.
Akizungumza na jijini Dar es Salaam, Madee alisema alikuwa amepanga kumtaka Dogo Janja aombe radhi kupitia vyombo vya habari na akanushe maneno aliyoyasema dhidi yake, lakini kwake ikawa ngumu.
“Dogo Janja alimuomba kwanza Mkubwa Fela na Babu Tale, wakaniambia kuhusu kurejea Tip Top, nikawaambia kitu gani nataka azungumze na waandishi kwa sababu hakuwahi kufanyiwa mambo aliyoyasema kwani alichokuwa ametaka ni kuwa chini ya mtu mwingine.
Hata hivyo, Madee alisema baada ya kukaa na uongozi wa kundi waliona kufanya hivyo itakuwa ni kudhalilishana tena, lakini pia Dogo Janja alisema yote aliyoyasema ilitokana na umri wake kuwa mdogo.
Aliongeza kutokana na yeye kuwa mshika dini mzuri na huu ni mwezi mtukufu, aliamua kumsamehe na kufungua ukurasa mpya wa maisha kwa manufaa ya msanii huyo na tasnia ya muziki.
“Kwahiyo sasa hivi tuko naye Tip Top, hatutaki kuyaongelea yale yaliyopita, tunataka tufunike kombe ili tuendelee na maisha mengine,” alisema.

No comments: