Monday 14 July 2014

Scolari aacha kazi baada ya Brazili kushindwa kufanya vyema katika michuano ya kombe la dunia

Scolari amelaumiwa kwa kichapo ilichopata Brazil
Ripoti nchini Brazil zinasema kuwa kocha wa timu ya taifa ya Brazil,Luiz Felipe Scolari, ameacha kazi kama meneja wa timu hiyo.
Scolari alilaumiwa pakubwa sana kwa timu ya Brazil kupata kichapo kibaya ilipocheza na Ujerumani ambao wameibuka mabingwa wa kombe la dunia mwaka huu.
Kichapo hicho kilikuja wakati wa mechi ya nusu fainali dhidi ya Ujerumani.
Taarifa rasmi huenda ikatolewa baadaye leo na shirikisho la soka la Brazil.

No comments: