Wednesday 23 July 2014

Israel yaua watoto wenyine kwa Bomu

UN: Israel inaua watoto na kubomoa hospitali GhazaMashirika ya Umoja wa Mataifa yamesema utawala haramu wa Israel umeua idadi kubwa ya watoto na kubomoa mahospitali katika mashambulizi yake ya kinyama yanayoendelea katika Ukanda wa Ghaza. Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa UNICEF imetoa taarifa hiyo na kuongeza kuwa, baada ya kupita wiki mbili za mashambulizi ya Israel huko Ghaza, asilimia 33 ya waliouawa shahidi katika mashambulizi hayo ni watoto. Msemaji wa UNICEF Christopher Tidey amesema, kwa ujumla hadi sasa Israel imeshaua watoto 121 wa Kipalestina katika Ukanda wa Ghaza na kwamba watoto waliojeruhiwa ni zaidi ya 904. Jumla ya Wapalestina waliouawa shahidi katika mashambulizi ya Israel huko Ghaza ni zaidi ya 610 huku wengine wasiopungua 3,600 wakijeruhiwa. Aghlabu ya wahanga wa mashambulizi hayo ya Israel ni raia wasio na hatia wakiwemo wanawake na watoto. Wakati huo huo, vituo vya afya vipatavyo 18 vimeharibiwa Ghaza, huku wahudumu 20 wa afya wakijeruhiwa wakati mashambulizi ya Israel dhidi ya Wapalestina yakiendelea. Shirika la Afya Duniani, WHO, limesema kuwa limesikitishwa mno na kuongezeka kwa mashambulizi dhidi ya vituo vya afya katika hujuma za utawala haramu wa Israel dhidi ya Ghaza. WHO imesema wahudumu wa afya ni lazima walindwe wakati wote, na kuruhusiwa kufanya kazi zao. Fadella Chaib kutoka WHO amesema kuwa, idadi kubwa ya majeruhi imezidi uwezo wa vituo vya afya ambavyo awali vilikuwa vikitoa huduma kwa hali ya kawaida. Katika hujuma yake Ghaza, Utawala wa Kizayuni wa Israel mbali na kuwaua watoto na kubomoa mahospitali pia unatumia silaha za maangamizi ya umati zilizopigwa marufuku duniani. Vitendo hivyo vyote vya Israel ni kinyume cha sheria za kimatiafa na ni jinai za vita lakini madola ya Magharibi yanayoongozwa na Marekani si tu kuwa hayalaani jinai hizo bali yanaunga mkono Israel na kuipa kinga isichukuliwe hatua za kisheria.

No comments: