Thursday 4 June 2015

Wanasiasa wa Tanzania waonywa utumiaji wa "Uchawi na viungo vya albino" katika Uchaguzi

Matumizi ya "Uchawi"  kuonywa katika Uchaguzi TanzaniaWanasiasa wa Tanzania waonywa utumiaji wa "Uchawi na viungo vya albino" katika Uchaguzi

Wanasiasa nchini Tanzania wameonywa kushiriki katika utumiaji wa uchawi katika uchaguzi wa mwaka 2015.
Kwa taarifa iliyotolewa kuhusu bunge la kutunga sheria, kuhusika na wimbi la mashambulizi dhidi ya albino ambapo sehemu ya mwili wake umekuwa ukiuzwa katika soko la Uchawi.
Naibu Waziri wa mambo ya ndani Perira Silima, alisema kuwa tuhuma za wanasiasa kuhusika na mauaji ya albino inaweza kuwa kweli kufuatia kufufuka kwa mashambulizi mapya dhidi ya albino mara baada ya mchakato wa  uchaguzi kuanza.
Silima, aliwataka wanasiasa kutokuamini ahadi wanazopewa na waganga wa kienyeji.
Baadhi ya wanasiasi huamni ahadi wanazopewa kuhusu ushindi katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika nchini Tanzania ifikapo mwezi Oktoba.
Perira, alisema kuwa "Nataka kuwahakikishia wanasiasa wenzangu kwamba hakutakuwa na kiti chochote bungeni ambacho kitachukuliwa kutokana na utumiaji wa viungo vya mwili wa albino"

No comments: