Tuesday 24 June 2014

Algeria yaandika historia, yaifunga Korea 4-2

Algeria yaandika historia, yaifunga Korea 4-2Algeria imebadili historia na kuwa timu ya kwanza kutoka barani Afrika kushinda magoli manne katika fainali za kombe la dunia. Algeria iliifunga Korea Kusini jumla ya magoli 4-2.

Ilichukua dakika 26 tu kwa Algeria kupata goli lake la kwanza kupitia kwa Slimani kabla ya Halliche kutia goli la pili kimyani dakika mbili mbele. Haikuchukua muda mrefu zaidi kabla ya kupata goli la tatu katika dakika ya 38.
Kipindi cha pili kilikuwa na mikikimikiki mingi zaidi. Korea walijaribu kupunguza magoli na kupata goli la kwanza katika dakika ya 50. Hata hivyo Algeria walizidisha wimbi la magoli kwa kufunga goli katika dakika ya 62. Dakika ya 72 Korea walipata goli la pili na la mwisho.

No comments: