Sunday 22 June 2014

Polisi nchini Kenya kuishi kwa pamoja

KITENGO cha utendaji kazi cha askari polisi nchini Kenya kimekumbwa na ukosefu wa makazi.

Hali imekuwa mbaya zaidi katika siku za hivi karibuni kiasi kwamba maafisa wa kike na kiume wanalazimika kutumia kwa pamoja vyumba vyao vichache.

Hali hiyo imetokea baada ya zaidi ya maafisa wapya 7,000, kuingizwa katika kitengo hicho miezi miwili iliyopita na kuongeza idadi ya maafisa wa polisi nchini Kenya kwa asilimia 10.

Kwa mujibu wa BBC, hali inaweza kudorora zaidi mwaka ujao ikiwa vyumba vipya havitapatikana kwa haraka.

Maafisa wengine 10,000 wataapishwa kujiunga na idara ya polisi kuwatumikia wananchi na kulinda usalama.

Mpango huo wa kupanua kitengo hicho, ulizinduliwa Bungeni na katibu wa fedha, Henry Rotich, alipoisoma bajeti ya 2014/2015, juma lililopita.

Katika taarifa ya makamanda wa majimbo iliyooneshwa kwa waandishi wa habari, maafisa waliamrishwa kuwakaribisha wenzao wapya katika vyumba vyao wanamoishi pamoja na familia zao.

No comments: